PESA ZAWATOKEA PUANI

TAKUKURU Mkoa wa Kagera kwa kushirikiana na ofisi ya mashitaka ya Taifa Mkoa wa Kagera leo Agosti 3, 2020 inakusudia kuwafikisha katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Bukoba watu kumi na moja kujibu mashitaka ya Rushwa, uhujumu uchumi na utakatishaji wa fedha haramu wa zaidi ya shilingi milioni mia tisa (Shs 900,000,000/=).

Ndugu wanahabari,

Watu wanaotarajiwa kufikishwa mahakamani siku ya leo ni pamoja na;-

Prospery Kashangaki Murungi ambaye ni mkazi wa Karagwe na amewahi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya ya Chama Kikuu cha Ushirika cha wilaya ya Karagwe -KDCU LTD

Anna Michael Mlay ambaye ni mkazi wa Kyera- Mbeya aliyekuwa Meneja Utumishi na Utawala KDCU LTD

Sylvery Njagi –Mkazi wa Kaisho-Kyerwa ambaye amewahi kuwa Mkaguzi Mkuu wa ndani KDCU LTD

Justin Tinkaligaile Fidelis – Mkazi wa kata ya Nyakahanga Karagwe

Cyril Tambala Protase-Mkazi wa Rwabere –Kyerwa

Adriani Rwechungura Kabushoke –mkazi wa Rugu Karagwe

Sylvester Joseph Mugishagwe Mkazi wa Dar es Salaam na mfanyakazi wa Kampuni ya DAN CONSTRUCTION (T) LTD

Nestory Tiibaza huyu ni Mhandisi Mhandisi TARURA Nzenga - aliwahi kuwa Mtumishi katika ofisi ya RAS Kagera

Emanuel Ndyamukama huyu ni Mhandisi TARURA DSM - aliwahi kuwa Mtumishi katika ofisi ya RAS Kagera

Desderius Rutakyamirwa Mkazi wa Dar es Salaam na mfanyakazi wa Kampuni ya DAN CONSTRUCTION (T) LTD

Josephati Kinyina –mkazi wa Nyabiyonza Karagwe




Post a Comment

Please Select Embedded Mode To Show The Comment System.*

Previous Post Next Post

Disqus Shortname

sigma2

Contact Form