TAKUKURU Mkoa wa Kagera kwa kushirikiana na ofisi ya mashitaka ya Taifa Mkoa wa Kagera leo Agosti 3, 2020 inakusudia kuwafikisha katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Bukoba watu kumi na moja kujibu mashitaka ya Rushwa, uhujumu uchumi na utakatishaji wa fedha haramu wa zaidi ya shilingi milioni mia tisa (Shs 900,000,000/=).
Ndugu wanahabari,
Watu wanaotarajiwa kufikishwa mahakamani siku ya leo ni pamoja na;-
Prospery Kashangaki Murungi ambaye ni mkazi wa Karagwe na amewahi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya ya Chama Kikuu cha Ushirika cha wilaya ya Karagwe -KDCU LTD
Anna Michael Mlay ambaye ni mkazi wa Kyera- Mbeya aliyekuwa Meneja Utumishi na Utawala KDCU LTD
Sylvery Njagi –Mkazi wa Kaisho-Kyerwa ambaye amewahi kuwa Mkaguzi Mkuu wa ndani KDCU LTD
Justin Tinkaligaile Fidelis – Mkazi wa kata ya Nyakahanga Karagwe
Cyril Tambala Protase-Mkazi wa Rwabere –Kyerwa
Adriani Rwechungura Kabushoke –mkazi wa Rugu Karagwe
Sylvester Joseph Mugishagwe Mkazi wa Dar es Salaam na mfanyakazi wa Kampuni ya DAN CONSTRUCTION (T) LTD
Nestory Tiibaza huyu ni Mhandisi Mhandisi TARURA Nzenga - aliwahi kuwa Mtumishi katika ofisi ya RAS Kagera
Emanuel Ndyamukama huyu ni Mhandisi TARURA DSM - aliwahi kuwa Mtumishi katika ofisi ya RAS Kagera
Desderius Rutakyamirwa Mkazi wa Dar es Salaam na mfanyakazi wa Kampuni ya DAN CONSTRUCTION (T) LTD
Josephati Kinyina –mkazi wa Nyabiyonza Karagwe
Tags
BREAKING NEWS