Mwanamuziki Yahaya Sharif-Aminu (22) amehukumiwa kunyongwa hadi kufa kwa kosa la kumkashifu Mtume Muhammad kupitia wimbo alioutoa Machi 2020. Sharif-Aminu hakukana mashtaka dhidi yake. Hata hivyo jaji amesema ana nafasi ya kukata rufaa dhidi ya hukumu hiyo.