Kufuatia semina iliyokuwa imeanza katika usharika wa KKKT Kijitonyama ikiongozwa na Rev Dr. Eliona Kimaro imelazimika kusimama kufuatia barua aliyopewa ya likizo ya siku 60 na kupelekea kushindwa kuendelea na semina hiyo na rasmi jana ameaga usharika wa KKKT Kijitonyama.
Mchungaji Kimaro amesema anatumia fursa hiyo kuwaaga usharika wa KKKT Kijitonyama na kuanzia kesho (yaani leo) Mchungaji Anna ataendelea kuwa Mchungaji wa Kanisa hilo, alisema Mchungaji Eliona Kimaro.
"Mimi ni Mchungaji wa Lutheran ninaye heshimu kiapo changu cha kichungaji na kuishi katika kiapo changu cha kichungaji na maadili pia ya kichungaji kwa neema ya Mungu. Kwa sababu hiyo imenilazimu kutii amri na kwenda kwenye hiyo likizo ya siku 60 na baadae kuripoti kwenye ofisi ya Askofu kama nilivyo elekezwa asante" alisema