Maelfu ya wananchi wanaopinga Serikali wameandamana kwa mara nyingine wakimtaka Rais wa nchi hiyo Ibrahim Boubacar Keita kujiuzulu
Licha ya mvua kunyesha, waandamanaji walikusanyika katika Mji Mkuu wa nchi hiyo, Bamako kushinikiza Rais aachie madaraka wakimlaumu kwa masuala mbalimbali ikiwemo ufisadi
Maandamano hayo yamefanyika ni ya kwanza kufanyika tangu Julai baada ya kundi la wapinzani kuingia makubaliano ya muda katika kampeni yao ya kumuondoa Rais Keita madarakani
Hali hiyo imetokea licha ya Rais wa zamani wa Nigeria ambaye pia ni Mpatanishi wa ECOWAS, Goodluck Jonathan kuwasihi wapinzani kuepuka maandamano na kufanya mazungumzo.
Tags
UCHAGUZI