.“Tunatuma fedha za Bodi ya Mfuko wa Barabara (Road Fund) na tunatuma fedha za
Halmashauri haiwezekani Barabara mbovu Kusini -DSM, hakuna stendi Somanga,
Uchaguzi unakuja, tujipange vizuri na tuchague wawakilishi ambao tutawabana na
watatuwakilisha vizuri “Kwa mujibu wa Sheria ya Barabara, Barabara ikishakua ya
lami inapata 100% ya ukarabati (Maintanance), Fedha za Bodi ya Mfuko wa Barabara
(Road Fund) sijui zinakwenda wapi!, Serikali haijalala, hili la ubovu wa
Barabara (Kusini-DSM) nawahakikishia nitalishughulikia mwenyewe”. “Kazi
aliyoifanya Mkapa ameifanya kwa nguvu zote, nawaomba wananchi wa kusini tumuenzi
Mkapa kwa kuchapa kazi, tuna eneo zuri mno, ufuta unakubali, mahindi, korosho
vyote vinakubali, na mifugo inakubali, tuchape kazi na tupendane, Kero ya
Barabara (Kusini-DSM) hii nimeibeba” “Barabara hii ya Mtwara - Lindi-Dar es
salaam imeharibika sana, Waziri wa Ujenzi atafute utatuzi wa hii Barabara,
ajipange vizuri utunzaji sio mzuri”-JPM njiani kuelekea DSM ,Ilibidi niende Dar
es Salaam kwa kutumia Ndege kutokea Mtwara lakini nimepita hii Barabara (Mtwara-
DSM) makusudi nione hali yake, hii Barabara imeharibika, 90 KM zote
zimeharibika. magari yenye uzito mkubwa yameharibu hii Barabara”-JPM njiani
kuelekea DSM
Tags
BREAKING NEWS