KUFUATIA KIFO CHA MKAPA: BENDERA ZA KENYA KUPEPEA NUSU MLINGOTI
Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta ametangaza siku 3 za maombolezo ya Kitaifa nchini humo na bendera zitapepea nusu mlingoti kuanzia Julai 27 - Julai 29 kufuatia kifo cha Rais Mstaafu wa Tanzania, Benjamin Mkapa
Amesema, "Bendera ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Bendera ya Kenya zitapepea nusu mlingoti. Bendera ya Kenya itafanya hivyo kwenye majengo yote ya Serikali pamoja na Balozi zake"
Ameongeza kuwa hiyo ni ishara ya heshima na shukrani kwa jukumu kubwa ambalo Mkapa alichukua katika kukuza mshikamano ndani ya Taifa lao, na kwa kuzingatia heshima kubwa aliyonayo katika Taifa la Kenya
Amesema, "Kenya tutashukuru milele kwa jukumu muhimu lililochezwa na Marehemu Rais Mkapa katika mchakato wa upatanishi uliomaliza vurugu za baada ya Uchaguzi na machafuko ya kisiasa 2007/08"
Amesisitiza, "Amani ya Taifa letu, maridhiano na umoja mkubwa unaweza kuhusishwa moja kwa moja na vitendo, hekima, upatanishi na kujitolea kwa Rais na Marehemu Mkapa na wenzake"
Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta ametangaza siku 3 za maombolezo ya Kitaifa nchini humo na bendera zitapepea nusu mlingoti kuanzia Julai 27 - Julai 29 kufuatia kifo cha Rais Mstaafu wa Tanzania, Benjamin Mkapa
Amesema, "Bendera ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Bendera ya Kenya zitapepea nusu mlingoti. Bendera ya Kenya itafanya hivyo kwenye majengo yote ya Serikali pamoja na Balozi zake"
Ameongeza kuwa hiyo ni ishara ya heshima na shukrani kwa jukumu kubwa ambalo Mkapa alichukua katika kukuza mshikamano ndani ya Taifa lao, na kwa kuzingatia heshima kubwa aliyonayo katika Taifa la Kenya
Amesema, "Kenya tutashukuru milele kwa jukumu muhimu lililochezwa na Marehemu Rais Mkapa katika mchakato wa upatanishi uliomaliza vurugu za baada ya Uchaguzi na machafuko ya kisiasa 2007/08"
Amesisitiza, "Amani ya Taifa letu, maridhiano na umoja mkubwa unaweza kuhusishwa moja kwa moja na vitendo, hekima, upatanishi na kujitolea kwa Rais na Marehemu Mkapa na wenzake"
Tags
BREAKING NEWS