"Ukweli ni kwamba wajumbe wa Zanzibar waliopiga kura ni 68. Kura walizopata wenzangu jumla ni 35. Sasa kutoka 68 kuna kura 33 za Zanzibar zilizokuja kwangu, na hiyo ni kwa kudhania hao wenzangu hawajapata kura hata moja toka Bara, jambo ambalo si sahihi." "Mimi nimekuwa Mbunge katika Jimbo la Kwahani Zanzibar kwa kipindi cha miaka 15. Miaka 15 ni mingi, na kusema kwamba mtu sifahamiki ilikuwa si sahihi." - Mgombea Urais Zanzibar kupitia CCM, - Dkt Hussein Mwinyi.
Tags
BREAKING NEWS