RAIS CHAKWERA ASEMA AFRIKA HAITAKIWI KUTEGEMEA MISAADA KUTOKA ULAYA

Rais wa Malawi, Dkt. Lazarus Chakwera amesema ifike wakati Afrika ifanye chaguzi zake kwa kujitegemea wenyewe bila kualika waangalizi kutoka nje ya bara hilo. Amesema mara nyingi waangalizi wanaokuja Afrika huandika yale wanayoyataka wao, na wakati mwingine huwa si sahihi.



“Lazima tufanye Chaguzi zetu bila Waangalizi wa Kimataifa kwasababu wao wakija huwa wanatoa taarifa zao wenyewe wanazoamua kuzitoa, Afrika inaweza kuimairisha Demokrasia yake yenyewe, tuchukue jukumu letu na sio kusubiri wengine”-Chakwera mbele ya JPM



“Kaka yangu Magufuli ameniambia Malawi tusijifikirie kama tuko mbali na Bahari tunaweza kuifikia Bahari kupitia Bandari ya DSM na Mtwara, pia ameniambia mkataba wowote tunaotakiwa kuusaini tutausaini, tumewaagiza Watendaji wetu waiandae mikataba hiyo” -Chakwera




Post a Comment

Please Select Embedded Mode To Show The Comment System.*

Previous Post Next Post

Disqus Shortname

sigma2

Contact Form