Mratibu wa Bima ya Afya ya CHF iliyoboreshwa Mkoa wa Dodoma Dkt.Francis Lutalala amesema kwa Mkoa wa Dodoma Serikali imefanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya Afya ili wananchi wakiwemo wazee wapate huduma za Afya kwa gharama nafuu hkvyo kusisitiza wananchi kujiunga na Bima CHF
“Tunaendelea na jitihada kuhakikisha wazee nchini tunawatambua na kuwapatia vitambulisho vitawawezesha kupata huduma za Afya bure na ninashukuru kwa kuwa Mkoa wa Dodoma unaongoza kwa hilo, ,hongerni sana”Dkt.John Jingu,Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii
Zaidi ya Wazee Milion moja kati ya Milioni mbili na laki tano nchi nzima wamekwisha patiwa vitambulisho vitakavyowawezesha kupata huduma za Afya Bure huku Mkoa wa Dodoma Ukiongoza kwa asilimia 76,Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii, Dkt.John Jingu amesema

